Kiswahili Language Version of "Top 10 Myths About Civil Society Participation at ICANN"

Robin Gross robin at IPJUSTICE.ORG
Tue Sep 15 23:13:51 CEST 2009


Thank you, Alex and Muting'u!   This is certainly a first for NCUC  
and I hope it will help us to reach many more people in East  
Africa.   Thanks for your work to make that happen!

Best,
Robin


On Sep 15, 2009, at 12:05 PM, Alex Gakuru wrote:

> Hi Robin, all,
>
> Grace Muting'u has kindly translated the document into Kiswahili
> (spoken by at least 120 million people in East African Community
> member countries alone).
>
> Asante (Thanks) Grace.
>
> Regards,
>
> Alex
>
> ---begins----
> “Porojo Kumi maarufu zaidi  kuhusu uhusikaji wa mashirika ya shirika
> la ICANN”, na NCUC
>
> 21 Agosti 2009
> ______________________________________________________________________ 
> _______
> Porojo ya Kwanza
>
> “Masirika ya kijamii hayatahusika kwenya ICANN chini ya mpango
> uliopendekezwa na NCUC.”
>
> Uwongo: Wafanyakazi wa ICANN na wengine wanadai kwamba
> mashirika  ya  kijamii hukatwa tamaa yasijihusishe na ICANN
> kwa vile mpango uliopendekezwa na ICANN hauhakikishi kwamba
> viti katika Kamati ya GNSO vitagawiwa maeneo au washikadau wote.
>
> Ukweli wa mambo ni kwamba uanachama wa NCUC unawakilisha
> mashirika 143 yasiyo ya kibiashara pamoja na watu binafsi. Tangu
> mwaka 2008 uanachama wa NCUC umeongezeka kwa zaidi ya 215%
> - hii ni kwa mujibu wa mwito wa mashirika ya kijamii. Hakuna shirika
> hata moja lisilo la kibiashara lililotoa maoni kwamba kuwepo tu kwa
> viti vya maeneo katika Kamati ya GNSO ndipo kungewafanya kushiriki
> kwenye ICANN. Katika mashirika yaliyotoa maoni yao, hakuna
> lilisosema ya kwamba lingeshiriki kwenye ICANN sharti katiba ya
> NSCG ingewahakikishia kiti kwenye Kamati ya GNSO.
>
> Porojo ya Pili
>
> “Wengi zaidi kutoka mashirika ya kijamii watashiriki kwenye ICANN
> Bodi itakapoingilia”
>
> Picha ya kweli: Kulazimisha kwa Bodi kwa katiba yake au kutosikiliza
> kwa Bodi kwa vikundi vya mashirika ya kijamii kutaonekana kama
> kukataliwa kwa maoni ya vile vikundi vingi vilivyoonelea kwamba ni hii
> ni dhuluma dhidi ya mashirika ya kijamii. Sifa ya ICANN kati ya
> mashirika yasiyo ya kibiashara itaharibika kabisa hatua mwafaka
> isipochukuliwa au suluhu kupatikana. Hata kama vitendo hivyo
> vingekubalika, matokeo  kamili kwa wafanya kazi na kwa katiba
> ya NCSG itakuwa kuvinyima nguvu vikundi visivyo vya kibiashara
> na kuvifanya hata visipende kushiriki. Kuteuliwa kwa waakilishi na
> Bodi hufurutisha  vikundi visivyo vya kibiashara na watu binafsi.
> Isitoshe, SIC inayowakilisha maeneo au washika dau wote inahitaji
> fedha nyingi sana ambayo mashirika mengi yasiyo ya kibiashara
> hayawezi kusimamilia. Pia, mpangilio huo utaleta mgawanyiko kati
> ya vikundi huku vikipigania wanachama na kura. Vikundi vingi visivyo
> vya kibiashara havitaweza kuingia ICANN GNSO chini ya mpango huo.
>
> Porojo ya Tatu
>
> Kuwepo kwa upinzani kunaweza kupuuzwa tu kama “kampeni ya
> uandikaji barua”
>
> Hii ni shutma isiyo ya kweli: Upinzani mkali wa mashirika ya kijamii
> kwa katiba ya SIC ulitokea si mara moja bali mara mbili. Pia, kulikuwa
> na ongezeko kubwa la wanachama wa NCUC lililotokana na kutopendezwa
> kwa jamii yote kwa jumla na vitendo vya wafanyakazi pamoja na Bodi.
> Kujaribu kupunguza ushiriki wa mashirika ya kijamii hakutafanikiwa na
> kunaonyesha upotovu huu wa hali ya juu. ICANN inahitajika kuwa na
> nyakati za maoni ya umma kwa maana ni lazima isikize na kujibu
> maswala ya jamii. Maoni ya umma hutokana na kuwepo kwa mawasiliano
> na mazungumzo kuhusu hata maswala tata, hata kama ni  miito ya
> kuchukua hatua. Hakuna mpango au sheria inayoipa ICANN au
> wafanyakazi wake uwezo wa kuamua kutotilia maanani au kupuuza
> vikundi karibu vyote vilivyoonyesha kutaka kushiriki kwenye  
> marekebisho
> ya GNSO, eti kwa sababu wamewashutumu wafanyakazi wa ICANN.
>
> Jaribio la ICANN la kutaja maoni haya ya muhimu kama “kampeni ya
> uandikaji barua” inapuuza ushiriki wa siku zijazo na imani katika
> mipango ya ICANN ya kuhusisha umma.
>
> Porojo ya Nne
>
> "Mashirika ya kijamii yamegawanyika kuhusu swala la katiba ya NCSG."
>
> Si Kweli. Hakujawahi kuwa na maoni ya umma yaliyoegemea upande mmoja
> kama haya katika historia ya ICANN. Hata kama wafanyikazi wa ICANN
> wanaiambia Bodi kwamba mashirika ya kijamii yamegawanyika, maoni zaidi
> yanakataa katiba iliyopendekezwa na ICANN na kuiunga mkono
> iliyopendekezwa na NCUC. Wanabodi wanaotegemea habari kutoka kwa
> wafanyikazi wa ICANN pekee wanaweza kuamini kwamba mashirika ya
> kijamii yamegawanyika , lakini wanabodi ambao wanesoma maoni ya umma
> wanaweza kuona umoja wa mashirika ya kijamii katika kupinga  
> kulazimishwa
> kufanya ICANN inavyotaka.
>
> Porojo ya Tano
>
> "Mashirika ya Kijamii yaliyoko kwa sasa hayawakilishi kamili  
> washikadau wote"
>
> Si kweli kwa vyovyote. Kwa sasa, kikundi cha mashirika ya kijamii,
> kijulikanacho
> kama NCUC kina wanachama 143 ambao kati yao 73 ni mashirika yasiyo ya
> kibiashara na watu banafsi 70 kutoka nchi 48. Hili ni ongezeko la  
> 215% tangu
> kanuni  ya uakilishaji wa wote ianzishwe.
>
> Ushiriki wa jamii isiyo ya kibiashara umeongezeka na kwa hivyo si  
> haki kusema
> kusema kwamba NCUC haishirikishi washika dau wote bila ya kusema  
> hivyo juu
> ya jamii zingine. Hata mwaka wa 2006, utafiti huru uliofanywa na  
> London School
> of Economics ulionyesha kuwa NCUC iliwakilisha maeneo mengi zaidi  
> na pia
> ilikuwa na watu wengi zaidi tofauti katika kamati ya GNSO wakati  
> wowote, na
> kwamba ilibadilisha zaidi wawakilishi wake katika kamati hio  
> ikilinganishwa na
> jamii zile zingine sita.
>
> Kwa upande mwingine, jamii ya wanabiashara imekuwa ikiwakilishwa na  
> watu
> wale wale 5 kwa Kamati kwa muongo mmoja na kulipokuwa na mwito wa
> marekebisho ya GNSO, 3 kati ya wanakamati 6 wa jamii ya kibiashra
> watawakilisha Marekani.
>
> Porojo ya Sita
>
> “ALAC inapendelea mkataba uliopendekezwa na wafanyakazi wa ICANN
> kuliko ule wa mashirika ya kijamii”
>
> Uwongo: Kiongozi mmoja wa ALAC alisema kuwa anapendelea maktaba
> uliopendekezwa na wafanyikazi. Wafanyikazi walichukua msemo huo na
> kuupeleka kwa Bodi ya ICANN huku wakidai kwamba ALAC inapendelea
> mkataba uliopendekezwa na wafanyikazi wa ICANN. Kwa kweli, taarifa
> rasmi iliyotolewa na ALAC na iliyopitishwa na na ALAC ilisema kuwa
> wanachama wengi wa ALAC waliunga mkono pendekezo la “kulitenganisha
> swala la viti vya Kamati kutoka kwa maeneo ni jambo nzuri na mwelekeo
> mwema.”
>
> Porojo ya Saba
>
> "Mkataba wa NCUC utakipa kikundi kile kile kidogo viti 6 badala ya 3"
>
> Uwongo:   Kwa miezi minane iliyopita, NCUC imekuwa ikitangaza kuwa
> itajitawanya muda tu NCSG itakapoundwa. Haina maana kuwa na “jamii ya
> mashirika yasiyo ya kibiashara” na vile vile “washika dau wasio wa
> kibiashara” kwani haya ni maneno yenye maana sawa. Kwa hivyo, viongozi
> wa NCUC hawatakuwa na uwezo wa kuendesha NCSG mpya – uongozi mpya
> utachaguliwa. Chini ya mkataba, mashirika na watu wote binafsi  
> watapiga
> kura kuchaga viti vya Kamati, na si tu wanachama wa hapo mbeleni wa
> NCUC. Masharti makali kuhusu uakilishi kutoka maeneo yote ya  
> kijografia
> yatamaanisha kuwa wanaowania kutoka maeneo yote duniani
>  watachaguliwa hata kama hawatapata wingi wa kura.
>
> Porojo ya Nane
>
> "NCUC haitagawana viti vya Kamati na jamii zingine za mashirika yasiyo
> ya kibiashara."
>
> Si Kweli: Mkataba wa NCUC uliundwa ili kuwezesha mashirika yasiyo ya
> kibiashara kuwa na wawaniaji wao wa viti vya Kamati. Ikilinganishwa na
> uwepo na uanachama wa NCUC, jamii nyingi zenye ajenda zinazoshindana
> zitajitokeza. Kukua kwa maeneo kutoka mashinani hadi juu ni bora
> kuliko mwelekeo wa Bodi/Wafanyikazi- pia unafanana zaidi na mapedekezo
> ya BGC. Maktaba wa SIC unaelekeza uundaji wa maeneo kutoka juu na hii
> ni ngumu na inaipa Bodi uwezo uliozidi kuamua “ushirikishaji” au
>  “umuhimu” wa washiriki wapya. Kwa vile uakilishi wa maeneo unategemea
> viti vya Kamati. Viti vya Kamati vikilinganishwa na maeneo, kila eneo
> litakuwa na mivurutano kuhusu kupewa kwa viti hivi vya Kamati
>
> Porojo ya Tisa
>
> "NCUC inataka kunyakua haki ya Bodi ya kupitisha maeneo”
>
> Uwongo: Watu wanaosema hivi ni dhahiri ya kwamba hawajasoma mkataba
> uliopendekezwa na NCUC. NCUC inapendekeza kwambo Bodi iwe na uwezo wa
> kupitisha au kukataza maeneo mapya yaliyoundwa chini ya mkataba huo.
>
> Pendekezo letu ni kuwe na na mielekezo ya kufuatwa (k.m nambari ya
> wagombea) kwa kuundwa kwa maeneo mapya halafu mapendekezo
> yatumwe kwa Bodi. Dhana ilikuwa kupunguza mzigo wa uundaji wa  
> maeneo mapya kwa
> wagombea na pia kwa Bodi.
>
> Mkataba uliopendekezwa na NCUC una mapendekezo rahisi sana ya kuunda
> maeneo mapya ukilinganishwa na ule wa SIC ambao utafanya uundaji wa
> maeneo mapya kuwa jambo gumu sana.
>
> Porojo ya Kumi
>
> “Azma ya kuwa na eneo ni kuwa na kiti kwenya Kamati ya  GNSO.”
>
> Uwongo:  wengine hudai kwamba viti vya Kamati ya GNSO lazima
> vilinganishwe kikamili na maeneo haswa kwa vile eneo halina maana bila
> kuhakikishiwa kiti kwenye Kamati ya GNSO. Lakini, kusema hivyo ni
> kutoelewa umuhimu wa maeneo katika GNSO mpya, ambao ni kuwapa sauti na
> namna ya kushiriki katika utengenezaji wa sera –wala si kuhakikishiwa
> kuwa na mjumbe asiye hata na mori wa kuafikiana na maeneo mengine.
>
> Viwili kati ya vikundi vitatu vya washikadau (Registries and  
> Registrars)
> vilipitisha mwelekeo wa mkataba wa NCUC wa kutenganisha
> viti vya GNSO kutoka kwa maeneo, walakini NCUC imekatazwa kuchagua
> wajumbe wake kulingana na SG.
>
> Ungana na NCUC
>
> Mashirika na watu wote binafsi kutoka jamii ya wasio wanabiashara
> wanaalikwa kuungana na NCUC kwenye mpango ya utengenezaji wa sera za
> GNSO ya ICANN. Leta maoni yako kwa mazungumzo ya sera za mtandao wa
> Internet na usaidie kulinda watumizi wa mtandao wasio wa kibiashara
> kwa kushiriki kwa ICANN kupitia kwa NCUC. Ingia leo kwa kwenda hapa:
>
> http://icann-ncuc.ning.com/main/authorization/signUp?
> ---ends----
>
> About Grace:
> =====================================================
> Grace Mutung’u (Bomu) is a young Kenyan lawyer who has been part of
> the Kenya ICT policy process since 2005. She works with theatre
> companies as an actor, marketer and cultural policy advocate. She is
> currently taking a course Intellectual Property Law and the Internet
> at Diplo Online Campus.
>
> Grace is a member of the ICT Consumers Association of Kenya.
> ====================================================<grace  
> mutungu.jpg>




IP JUSTICE
Robin Gross, Executive Director
1192 Haight Street, San Francisco, CA  94117  USA
p: +1-415-553-6261    f: +1-415-462-6451
w: http://www.ipjustice.org     e: robin at ipjustice.org



-------------- next part --------------
An HTML attachment was scrubbed...
URL: <http://lists.ncuc.org/pipermail/ncuc-discuss/attachments/20090915/f91b83c4/attachment.html>


More information about the Ncuc-discuss mailing list